manyaki-1.jpg ...      ...

Bashir amewasili mjini Khartoum Sudan

Rais Omar al Bashir wa Sudan amewasili mjini Khartoum Sudan kutoka nchini Afrika Kusini.
Rais Bashir amekariri kuwa hana hatia yoyote wala hajui kwa nini mahakama ya kimatiafa ya ICC inasisitiza kumchafulia jina.
Shirika la habari ya AFP limemnukuu rais Bashir akifoka ''Allah Akbar'' aliposhuka kutoka kwa ndege iliyombeba.
Aidha aliinua mkongojo wake juu na kushangiliwa na wafuasi wake.
Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Ibrahim Ghandour aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ya Afrika Kusini ilikuwa imemkariria rais Bashir kuwa kuwepo kwake mjini johannesburg ilikuwa ni tukio la kushabikiwa na lenye heshima kubwa kwa hivyo hakukuwa na uwezekano wowowte wake kukamatwa.
 Bashir amewasili mjini Khartoum Sudan
Rais Omar al Bashir wa Sudan amewasili mjini Khartoum Sudan kutoka nchini Afrika Kusini.
Rais Bashir amekariri kuwa hana hatia yoyote wala hajui kwa nini mahakama ya kimatiafa ya ICC inasisitiza kumchafulia jina.
Shirika la habari ya AFP limemnukuu rais Bashir akifoka ''Allah Akbar'' aliposhuka kutoka kwa ndege iliyombeba.
Aidha aliinua mkongojo wake juu na kushangiliwa na wafuasi wake.
Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Ibrahim Ghandour aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ya Afrika Kusini ilikuwa imemkariria rais Bashir kuwa kuwepo kwake mjini johannesburg ilikuwa ni tukio la kushabikiwa na lenye heshima kubwa kwa hivyo hakukuwa na uwezekano wowowte wake kukamatwa.
 Rais Bashir alipotua mjini Khartoum
Rais Huyo alikuwa ameratibiwa kuhutubia umma lakini kinasa sauti kikaharibika na akaondoka.
Rais Bashir aliingia katika gari lake lililo wazi na akaondoka uwanjani huku akishangiliwa na wafuasi wake.
Kuondoka kwake nchini Afrika Kusini kulikumbwa na hati hati, baada ya mahakama moja kuamuru rais huyo asiondoke nchini humo hadi mahakama hiyo itakaposikiliza kesi na kuamua iwapo atakamatwa na kupelekwa mjini the Hague Uholanzi au la.
Awali mwandishi wa BBC aliyeko Afrika Kusini Nomsa Maseko, alisema kuwa ndege ya rais al Bashir ilijazwa mafuta jana usiku na kuwekwa mstari wa mbele tayari kabisa kuondoka katika uwanja wa ndege wa kijeshi.
 Ndege iliyombeba rais Bashir ikiondoka Afrika Kusini 

Previous
Next Post »