manyaki-1.jpg ...      ...

KWA MARA YA KWANZA MISS TANZANIA KUFANYIKA MWANZA NDANI YA ROCK CITY MALL KIRUMBA 29 OCTOBER 2016

Baada ya kimya na mvutano wa hapa na pale kuhusu miss tanzania kwa kuponyoka kwa maadili na ubadilifu ukilinganisha na udanganyifu wa umri wa washiriki wa taji hilo,mpaka kufikia serikali kuingilia kati,sasa jiji la mwanza limeamua kuleta sura mpya ya taji hilo kwa kuamua kuleta kilele cha mashindano hilo kwa  mara ya kwanza jiji mwanza.
jiji la mwanza na viunga vyake leo vitasimama kwa mda usiku wa leo baada ya shindano hilo kufanyika katika ukumbi wa kisasa wa Rock city mall mwanza kirumba katika barabara ya Airport.jirani na villa pack resourt.
mratibu wa shindano hilo amesema kuwa viingilio vitakuwa kama ifuatavyo kawaida,20,000/= gold 50,000/= halafu VIP 100,000/=




Mashindano hayo kwa jiji la mwanza ambayo yatawakilisha warembo wote wa mikoa ya tanzania bara na visiwani watashiriki kwa kuwakilisha mikoa yao kwa lengo la kutwaa taji la umiss 2016/17 nje ya taji pia kuna zawadi ambazo zitatolewa.
shindano hilo limeletwa kwa udhamini wa JEMBENIJEMBE,ROCK CITY MALL NA BERMADAZ TV MWANZA.


Previous
Next Post »