manyaki-1.jpg ...      ...

BI AISHA MTUMWA:MKURUGENZI WA FARIJIKA ORGANIZATION AZUNGUMZIA MAANDALIZI YA TAMASHA LA CHAKULA CHA PAMOJA NA WATOTO YATIMA MWANZA 18 DECEMBER 2016


Mkurugenzi Mtendaji wa FARIJIKA COMMUNITY DEVELOPMENT AND RIGHT ORGANIZATION,Bi Aisha Mtumwa, Amesema kuwa  maandalizi ya tamasha la chakula cha pamoja na watoto yatima,walemavu na watoto waishio kwenye mazingira magumu wa mkoa wa mwanza pamoja na wadau mbalimbali yanaendelea vizuri baada ya kuendelea kupata support toka kwa watu mbalimbali.
Akizungumza mapema leo Bi Aisha amesema Tamasha hilo litafanyika tarehe 18.12.2016 Katika ukumbi wa Bwalo La Jeshi jirani na Mahakama ya Mwanzo karibu na mwanza Gardern kwa mkuu wa wilaya.
Pia bado ameendelea kuwapa fursa wadau wenye moyo wa kujitolea kujitokeza kwa wingi kuchangia michango mbalimbali hili kufanyikisha tamasha hilo.
Pia Bi Aisha ameendelea kutoa shukrani kwa Kituo Cha Barmedaz Tv Kwa kujitolea kurusha Tamasha hilo siku ya jumapili ya  18.12.2016.
mbali na barmedaz Tv pia vyombo mbalimbali vya habari vimealikwa kuhudhulia  tamasha hilo.
Kuendelea kujua mengi kuhusu  FARIJIKA COMMUNITY DEVELOPMENT AND RIGHT ORGANIZATION na yatakayojiri katika tamasha hilo usiache kutembelea Blog hii au kwa mawasiliano piga 0756-040261 kwa mawasiliano zaidi au kama utahitaji kuchangia.
Previous
Next Post »