ghasia katika barabara za Burundi
Muungano
wa Ulaya EU umeanza kikao maalum kujadili uwezekano wa kukata msaada
wake nchini Burundi. Inakisiwa kuwa fedha kutoka muungano huo unafikia
zaidi ya nusu ya bajeti nzima ya Burundi ya kila mwaka.
Upande wa uchaguzi ulisusia kura hiyo iliyofanywa siku ya Jumanne. Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa Ijumaa hii.
Uamuzi wa Rais Pierre Nkurunzinza kuwania urais kwa muhula wa tatu umetajwa kwenda kinyume na mkataba waliosaini mjini Arusha miaka kumi na tano iliyopita, ambao ulimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka mingi.
Juhudi kadhaa za kuleta upatanishi kati ya makundi hasimu zimeambulia patupu.
http://frankmanyaki.blogspot.com/