manyaki-1.jpg ...      ...

PROF JAY SASA AMEAMIA KWENYE SOKA MIKUMI

Mbunge wa Jimbo la Mikumi ambaye pia ni msanii wa Bongofleva Joseph Haule a.k.a Professor Jay bado anaendelea na harakati zake za kutumikia wananchi wake wa Jimbo la Mikumi kama alivyowaahidi katika kampeni zake za ubunge.

img-20161117-wa0035
Baada ya kuangahikia tatizo la maji jimboni kwake na kuhakikisha studio yake ya Mwanalizombe inahamia Mikumikwa ajili ya vipaji vya muziki vya jimboni humo, amegeukia upande wa soka na kuamua kuanzisha Ligi ambayo ameiita Professor Jay Cup.

img-20161117-wa0038
Ligi hiyo ambayo itashirikisha timu 32 kutoka katika kata 15 zaMikumi na kata za jirani, tayari Professor Jay ameanza kwa kukabidhi jezi, mipira na soksi kwa timu zote 32 zilizoomba kushiriki, Ligi itachezwa kwa mfumo wa nyumbani na ugenini na itaanza kwa weekend hii kuchezwa mchezo wa Ngao ya Hisani.
img-20161117-wa0040Mshindi wa kwanza wa Ligi hiyo atapewa zawadi ya Kombe kubwa na Tsh milioni 2, mshindi wa pili atapata Kombe dogo na Tsh milioni moja, mshindi wa tatu atapata Tsh laki saba na nusu wakati mshindi wa nne atapata Tsh laki tano, zikiambata na tuzo za mchezaji bora, kocha bora, golikipa bora na mfungaji bora.
Previous
Next Post »